Dirisha la Print litafunguka sasa. Chagua “Save as PDF” au “Print”.
Q-Zat Finance Limited
Vigezo na Masharti ya Huduma ya “Tunza”
Soma vigezo na masharti haya kwa utulivu. Ukishamaliza, jaza taarifa zako na usaini ili
kuchapisha au kusave PDF — ikiwa tayari imejazwa taarifa zako na sahihi zako.
Hati rasmi (PDF)
Sahihi za pande zote
Rekodi na uthibitisho
Vigezo na Masharti
Ada ya Usajili: TZS 1,800
Muhtasari wa Haraka (Kwa Uelewa wa Mteja)
Muhtasari huu ni wa kukusaidia kuelewa kwa haraka; maelezo kamili yako kwenye vipengele vilivyo hapa chini.
Huduma ya Tunza ni mpango wa kuweka akiba kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa, na fedha hutumika kukamilisha lengo la bidhaa lililochaguliwa.
Akaunti ya Tunza haitoi pesa taslimu; hakuna “withdraw” iniyoruhusiwa.
Hakuna marejesho ya pesa taslimu kwa hali yoyote; endapo mteja hatoweza kuendelea, anaweza kupewa bidhaa pekee inayolingana na salio lake kwa mujibu wa taratibu za huduma.
Mteja anaweza kuomba kubadilisha lengo; lengo jipya linapaswa kuwa na thamani sawa au kubwa kuliko lengo la sasa.
Utoaji wa bidhaa ni baada ya kukamilisha 100% ya lengo; maombi ya kuchukua kwa 75% huamuliwa kwa tathmini na yanahusu bidhaa za TZS 1,000,000 au zaidi, bila kuhusisha bidhaa za ofa.
Upatikanaji wa bidhaa hutegemea soko na wasambazaji; endapo bidhaa haitapatikana, inaweza kupendekezwa mbadala yenye thamani inayolingana.
Rekodi za Q-Zat ndizo hutumika kuthibitisha salio na historia ya malipo; mteja anashauriwa kuhifadhi kumbukumbu zake za miamala.
Q-Zat inaweza kuwasiliana na mteja kupitia simu, SMS, WhatsApp, barua pepe au App kwa taarifa muhimu za huduma na akaunti.
Q-Zat inaweza kusimamisha akaunti endapo kutabainika taarifa zisizo sahihi au matumizi yasiyo sahihi, na inaweza kuomba uthibitisho wa ziada kwa ajili ya usalama.
Kwa kuendelea na usajili na kuweka sahihi, mteja anakiri kuwa amesoma, ameelewa na amekubali vigezo na masharti ya huduma.
Hati hii inaeleza utaratibu, kanuni na masharti ya matumizi ya huduma ya Tunza inayotolewa na Q-Zat Finance Limited.
Lengo lake ni kumsaidia mteja kuelewa kwa uwazi jinsi huduma inavyofanya kazi, haki zake na wajibu wake.
1. Maelezo ya Huduma
Tunza ni huduma ya akiba ya malengo kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa.
Huduma humwezesha mteja kuweka akiba kidogo kidogo hadi kufikia thamani ya bidhaa anayohitaji.
2. Usajili na Ada
Mteja anajisajili kwa kutoa taarifa sahihi na zinazotambulika.
Ada ya usajili ni TZS 1,800.
Hakuna makato ya ziada kwenye akiba ya mteja, isipokuwa pale ambapo kutatolewa taarifa rasmi endapo kutahitajika mabadiliko ya kiutendaji au kisheria.
3. Matumizi ya Akaunti ya Tunza
Akaunti ya Tunza hutumika kwa manunuzi ya bidhaa pekee.
Hakuna utoaji wa pesa taslimu (withdraw) unaoruhusiwa kutoka kwenye akaunti ya Tunza.
Fedha zote zilizowekwa hutumika kukamilisha lengo la bidhaa lililochaguliwa.
4. Uchaguzi wa Lengo (Bidhaa)
Mteja huchagua bidhaa na kuanza kuweka akiba kulingana na uwezo wake.
Upatikanaji wa bidhaa utategemea hali ya soko na wasambazaji waliopo.
Endapo bidhaa haitapatikana, Q-Zat inaweza kupendekeza bidhaa mbadala yenye thamani inayolingana.
5. Kubadilisha Lengo
Mteja anaweza kuomba kubadilisha lengo (bidhaa).
Hairuhusiwi kubadilisha lengo kwenda kwenye bidhaa yenye thamani ndogo kuliko lengo la awali.
Lengo jipya linapaswa kuwa na thamani sawa au kubwa kuliko lengo la sasa.
6. Vigezo vya Kupata Bidhaa
Bidhaa hutolewa baada ya mteja kukamilisha malipo ya lengo lake kwa 100%, au kwa 75% pale ambapo Q-Zat itaona mteja amekidhi vigezo maalum vya kupata bidhaa kabla ya kukamilisha 100%.
Baada ya kukamilisha lengo (kwa 100% au kwa 75% kwa idhini ya kampuni), mteja anatakiwa kusubiri hadi masaa 72 ili kuruhusu maandalizi ya bidhaa na taratibu za utoaji/ufikishaji kukamilika.
Ndani ya kipindi hicho cha masaa 72, Q-Zat itafanya uthibitisho wa salio, maandalizi ya bidhaa, na kupanga utaratibu wa kukabidhi au kufikisha bidhaa kulingana na upatikanaji wa bidhaa na eneo la mteja.
Bidhaa itakabidhiwa au kufikishwa kwa mteja baada ya taratibu hizo kukamilika, na mteja ataarifiwa rasmi kupitia njia za mawasiliano zilizoidhinishwa na Q-Zat.
7. Mteja Kushindwa Kuendelea
Kwa kanuni za huduma ya Tunza, mteja anayeshindwa kuendelea na mpango hatarudishiwa fedha taslimu kwa hali yoyote; fedha zote zinawekwa kwa ajili ya kupata bidhaa.
Ombi la kurejeshewa fedha au kusitisha mpango litazingatiwa tu endapo mteja yupo katika hali maalum kama kifo, magonjwa sugu, ajali au hali nyingine nzito zilizothibitishwa.
Mteja anatakiwa kuwasilisha ombi rasmi la maandishi likieleza sababu na kuambatanisha uthibitisho unaokubalika.
Ombi hilo litafanyiwa kazi ndani ya siku 7 hadi 14 za kazi tangu kupokelewa.
Endapo ombi litakubaliwa, mteja atapewa bidhaa pekee inayolingana na salio lililopo kwenye akaunti yake ya Tunza; hakuna marejesho ya pesa taslimu.
8. Sera ya Kuchukua Bidhaa kwa 75%
Utaratibu wa kawaida: bidhaa hukabidhiwa baada ya kukamilisha malipo ya 100%.
Kufikisha 75% ya malipo hakuleti uhakika wa moja kwa moja wa kuchukua bidhaa.
Maombi ya 75% yataangaliwa kwa tathmini ya Q-Zat (historia ya ulipaji, nidhamu ya malipo, historia ya mikopo taasisi nyingine, na uaminifu wa taarifa).
Mpango wa 75% unatumika kwa bidhaa zenye thamani ya TZS 1,000,000 au zaidi pekee.
Bidhaa za ofa (OFAs) au bidhaa zilizo chini ya mpango maalum wa ofa hazihusishwi na utaratibu wa 75%.
Q-Zat hufanya uamuzi wa mwisho kuhusu maombi ya 75%.
Mteja atakayekabidhiwa bidhaa kwa 75% ataendelea kukamilisha salio lililobaki kwa mpangilio uliopo.
9. Rekodi na Uthibitisho wa Malipo
Rekodi za Q-Zat ndizo hutumika kuthibitisha salio na historia ya mteja.
Mteja anashauriwa kuhifadhi kumbukumbu zake za miamala.
10. Mawasiliano
Q-Zat inaweza kuwasiliana na mteja kupitia simu, SMS, WhatsApp, barua pepe au App.
Mawasiliano hutumika kutoa taarifa muhimu kuhusu akaunti na huduma.
11. Faragha na Usalama wa Taarifa
Taarifa za mteja huhifadhiwa kwa usalama na kutumika kwa madhumuni ya utoaji wa huduma.
Taarifa zinaweza kutumika kwa uthibitisho wa miamala na uendeshaji wa huduma ya Tunza.
12. Haki na Majukumu ya Q-Zat
Q-Zat inaweza kusimamisha akaunti endapo kutabainika matumizi yasiyo sahihi au taarifa zisizo sahihi.
Q-Zat inaweza kuomba uthibitisho wa ziada inapohitajika kwa usalama wa mteja na mfumo.
13. Mabadiliko ya Masharti
Masharti haya yanaweza kufanyiwa maboresho ili kuboresha huduma.
Mabadiliko yatatolewa taarifa kwa mteja kupitia njia rasmi.
14. Sheria Inayotumika
Huduma ya Tunza inaendeshwa kwa kuzingatia sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
15. Utatuzi wa Migogoro
Changamoto au mgogoro utaanza kutatuliwa kwa mazungumzo na maelewano.
Ikiwa haitapatiwa suluhisho, hatua za usuluhishi zitazingatiwa.
Endapo bado haitatatuliwa, suala litapelekwa kwenye mahakama zenye mamlaka nchini Tanzania.
Jaza taarifa za mteja na taarifa za lengo. Kisha saini mteja na msimamizi wa akaunti ili kuchapisha/kusave PDF.
Jaza Taarifa & Sahihi
Print / Save as PDF
Q-Zat Finance Limited
Hati Rasmi ya Vigezo na Masharti ya Huduma ya “Tunza” (Inasainiwa wakati wa usajili wa kwanza)