Q-Zat Finance Limited

Vigezo na Masharti ya Huduma ya “Tunza”

Soma vigezo na masharti haya kwa utulivu. Ukishamaliza, jaza taarifa zako na usaini ili kupata PDF safi ya kuchapisha au kushare — ikiwa tayari imejazwa taarifa zako na sahihi yako.

Vigezo na Masharti

Ada ya Usajili: TZS 1,800

Hati hii inaeleza utaratibu, kanuni na masharti ya matumizi ya huduma ya Tunza inayotolewa na Q-Zat Finance Limited. Lengo lake ni kumsaidia mteja kuelewa kwa uwazi jinsi huduma inavyofanya kazi, haki zake na wajibu wake.

1. Maelezo ya Huduma

  1. Tunza ni huduma ya akiba ya malengo kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa.
  2. Huduma humwezesha mteja kuweka akiba kidogo kidogo hadi kufikia thamani ya bidhaa anayohitaji.

2. Usajili na Ada

  1. Mteja anajisajili kwa kutoa taarifa sahihi na zinazotambulika.
  2. Ada ya usajili ni TZS 1,800.
  3. Hakuna makato ya ziada kwenye akiba ya mteja, isipokuwa pale ambapo kutatolewa taarifa rasmi endapo kutahitajika mabadiliko ya kiutendaji au kisheria.

3. Matumizi ya Akaunti ya Tunza

  1. Akaunti ya Tunza hutumika kwa manunuzi ya bidhaa pekee.
  2. Hakuna utoaji wa pesa taslimu (withdraw) unaoruhusiwa kutoka kwenye akaunti ya Tunza.
  3. Fedha zote zilizowekwa hutumika kukamilisha lengo la bidhaa lililochaguliwa.

4. Uchaguzi wa Lengo (Bidhaa)

  1. Mteja huchagua bidhaa na kuanza kuweka akiba kulingana na uwezo wake.
  2. Upatikanaji wa bidhaa utategemea hali ya soko na wasambazaji waliopo.
  3. Endapo bidhaa haitapatikana, Q-Zat inaweza kupendekeza bidhaa mbadala yenye thamani inayolingana.

5. Kubadilisha Lengo

  1. Mteja anaweza kuomba kubadilisha lengo (bidhaa).
  2. Hairuhusiwi kubadilisha lengo kwenda kwenye bidhaa yenye thamani ndogo kuliko lengo la awali.
  3. Lengo jipya linapaswa kuwa na thamani sawa au kubwa kuliko lengo la sasa.

6. Mteja Kushindwa Kuendelea

  1. Mteja anatuma ombi rasmi la kusitisha mpango.
  2. Hakutakuwa na marejesho ya pesa taslimu.
  3. Mteja atapewa bidhaa inayolingana na salio lililopo kwenye akaunti yake.
  4. Ombi la kusitisha litafanyiwa kazi ndani ya siku 7 tangu kupokelewa.

7. Sera ya Kuchukua Bidhaa kwa 75%

  1. Utaratibu wa kawaida: bidhaa hukabidhiwa baada ya kukamilisha malipo ya 100%.
  2. Kufikisha 75% ya malipo hakuleti uhakika wa moja kwa moja wa kuchukua bidhaa.
  3. Maombi ya 75% yataangaliwa kwa tathmini ya Q-Zat (historia ya ulipaji, nidhamu ya malipo, historia ya mikopo taasisi nyingine, na uaminifu wa taarifa).
  4. Mpango wa 75% unatumika kwa bidhaa zenye thamani ya TZS 500,000 au zaidi pekee.
  5. Bidhaa za ofa (OFAs) au bidhaa zilizo chini ya mpango maalum wa ofa hazihusishwi na utaratibu wa 75%.
  6. Q-Zat hufanya uamuzi wa mwisho kuhusu maombi ya 75%.
  7. Mteja atakayekabidhiwa bidhaa kwa 75% ataendelea kukamilisha salio lililobaki kwa mpangilio uliopo.

8. Rekodi na Uthibitisho wa Malipo

  1. Rekodi za Q-Zat ndizo hutumika kuthibitisha salio na historia ya mteja.
  2. Mteja anashauriwa kuhifadhi kumbukumbu zake za miamala.

9. Mawasiliano

  1. Q-Zat inaweza kuwasiliana na mteja kupitia simu, SMS, WhatsApp, barua pepe au App.
  2. Mawasiliano hutumika kutoa taarifa muhimu kuhusu akaunti na huduma.

10. Faragha na Usalama wa Taarifa

  1. Taarifa za mteja huhifadhiwa kwa usalama na kutumika kwa madhumuni ya utoaji wa huduma.
  2. Taarifa zinaweza kutumika kwa uthibitisho wa miamala na uendeshaji wa huduma ya Tunza.

11. Haki na Majukumu ya Q-Zat

  1. Q-Zat inaweza kusimamisha akaunti endapo kutabainika matumizi yasiyo sahihi au taarifa zisizo sahihi.
  2. Q-Zat inaweza kuomba uthibitisho wa ziada inapohitajika kwa usalama wa mteja na mfumo.

12. Mabadiliko ya Masharti

  1. Masharti haya yanaweza kufanyiwa maboresho ili kuboresha huduma.
  2. Mabadiliko yatatolewa taarifa kwa mteja kupitia njia rasmi.

13. Sheria Inayotumika

  1. Huduma ya Tunza inaendeshwa kwa kuzingatia sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

14. Utatuzi wa Migogoro

  1. Changamoto au mgogoro utaanza kutatuliwa kwa mazungumzo na maelewano.
  2. Ikiwa haitapatiwa suluhisho, hatua za usuluhishi zitazingatiwa.
  3. Endapo bado haitatatuliwa, suala litapelekwa kwenye mahakama zenye mamlaka nchini Tanzania.

Sehemu ya Sahihi iko upande wa kulia. Jaza jina, account number, kisha usaini ili kupakua PDF.

Jaza Taarifa & Sahihi

PDF itapakuliwa
Sahihi ya Mteja
Saini ndani ya box

Ukibonyeza “Pakua PDF Iliyosainiwa”, mfumo utatengeneza PDF yenye: jina kamili, namba ya simu, tarehe na sahihi yako.